Bodi ya Utalii Tanzania na Nugaz Event Planner Kufanya Tamasha la Utalii Tarehe 27-28 Oktoba, 2012. Kijiji cha Makumbusho Dar es Salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
ya Utalii Tanzania, Aloyce Nzuki (kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa
Kampuni ya Nugaz Antonio Nugaz bango la
taarifa za tamasha la Utalii linalotarajiwa kufanyika Dar es Salaam mwezi ujao
ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa tamasha hilo. Halfa hiyo ilifanyika Dar es
Salaam jana ambapo kampuni ya Nugaz ya Dar es Salaam itaandaa tamasha hilo kwa
uratibu wa TTB
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
ya Utalii Tanzania, Aloyce Nzuki (kushoto) akikafafanua jambo kwa waandishi wa
habari hawapo pichani Dar es Salaama jana kuhusu tamasha la Utalii
linalotarajiwa kufanyika Dar es Salaam mwezi ujao ikiwa ni jitihada za TTB
katika kuutangaza utalii wa ndani.Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya
Nugaz Antonio Nugaz inayoandaa tamasha
hilo chini ya uratibu wa TTB.
MAELEZO YA MKURUGENZI MWENDESHAJI WA BODI YA UTALII TANZANIA
DR. ALOYCE NZUKI KUHUSU TAMASHA LA UTALII (UTALII FESTIVAL) KWA WAANDISHI WA HABARI 24/09/2012.
Lengo la mkutano huu ni
kutambulisha rasmi Tamasha la aina yake hapa nchini.
Bodi ya Utalii Tanzania kwa
kushirikiana na Nugaz Event Planner tumeamua kuanzisha tamasha la Utalii
linalojulikana kama Tanzania Utalii
Festival litakalokuwa linafanyika kila mwaka. Kauli mbiu ya tamasha hii ni “Enjoy Nature Experience Culture”.
Tamasha hili litaanza rasmi
mwaka huu ambapo litafanyika tarehe 27-28 Oktoba kijiji cha Makumbusho na
litakuwa linaanza saa nne asubuhi hadi saa nne usiku.
Tamasha hili litahusisha
shughuli mbalimbali kama vile ngoma za asili za makabila yetu hapa nchini,
vyakula na vinywaji vya asili vya makabila mbalimbali, n.k. Aidha, tamasha hili litahusisha vikundi
mbalimbali kutoka katika mikoa yetu ya Tanzania Bara na Visiwani ambavyo vitakuwa
vinaalikwa kushiriki katika tamasha.
Katika tamasha hili kutakuwa
pia na usiku wa Utalii. Huu utakuwa ni
usiku maalum kwa wale watakaokuwa wameshindwa kuhudhuria tamasha wakati wa
mchana kutokana na sababu mbalimbali.
LENGO LA TAMASHA
Wazo la kuwa na tamasha hili
limetokana na hali halisi ya idadi ndogo ya watalii wa ndani yaani watanzania
wanaotembelea maeneo mbalimbali ya vivutio vya utalii. Hivyo Bodi ya Utalii Tanzania na Kampuni ya
Nugaz Event Planner tukakubaliana kuwa na tamasha hili kwa lengo la kuhamasisha
Utalii Tanzania hususani Utalii wa Ndani, lakini pia tunaamini litasaidia
kuongeza mapato ya serikali.
Tunapenda kuwaalika
watanzania wote kuhudhuria katika tamasha hili kwa kiingilio kidogo cha Tsh.
2000/=.
Hivyo kwa taarifa zaidi
kuhusu tamasha hili tunawaomba mtembelee tovuti hii.
No comments:
Post a Comment